Miss Utalii wa ndani Tanzania -SIA NDASKOI akiwasili katika shule ya msingi ya St Mary Tabata kwa ajili ya kuhamasisha Utalii wa ndani. Hii ni sehemu tu ya ziara zake katika uhamasishaji huo.
Baadhi ya wanafunzi wa St. Mary's wakitoa burudani kwa Miss Utalii wa ndani na timu iliyofuatana nae shuleni hapo kwa lengo la kuhamasisha Utalii wa ndani
Miss Utalii wa ndani akiongea na wanafunzi kuhusu umuhimu wa Utalii wa ndani, kushoto kwake ni Bw. Hans Warburg afisa mwakilishi wa Kampuni ya kitalii ya Pongo Safari ambaye pia alikuwepo kwenye msafara huo kama mdau
Kila mwanafunzi alitamani kumshika mkono Miss Utalii wa ndani wakati wakihamasisha utalii wa ndani shuleni hapo
Miss Utalii wa ndani Tanzania SIA NDASKOI (kushoto), Miss Tanzania 2009 MIRIAM GERALD (katikati) na Miss Tanzania namba tatu JULIETH WILLIAM (kulia) pamoja wakishirikiana kuzungumza na wanafunzi wa St. Mary's waakati wa ziara hiyo ya ma Miss katika harakati na mkakati kabambe wa kuhamashisha Utalii wa ndani
Miss Tanzania namba tatu 2009 JULIETH WILLIAM akionyesha jarida linalohusu vivutio vya Utalii Tanzania kwa wanafunzi wa St Mary's. Alikuwa katika msafara wa Miss Utalii wa ndani katika harakati zao za kuhamasisha Watanzania kutembelea vivutio vya Utalii nchini.